skip to main |
skip to sidebar
Zitto Kabwe na Maalim Seif wakutana Marekani
Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe na katibu mkuu wa
chama cha wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad wamekutana Katika
Mkutano Maalum wa Viongozi wa Kisiasa Ulimwenguni (International Leaders
Forum) ambao unafanyika leo Asubuhi ‘Kwa Saa za Marekani’ Jijini
Philadelphia.
Mkutano huo ulioandaliwa na asasi ya NDI ‘National Democratic
Institute’, ni Sehemu ya matukio maalum kuelekea Mkutano Mkuu wa Chama
Cha Democrats (Democratic National Convention), Mkutano ambao
utamthibitisha Bibi Hillary Clinton Kuwa Mgombea Urais Kupitia Chama
Hicho.
Zitto Kabwe Pamoja Na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim watakuwa Philadelphia
mpaka Siku ya alhamis ambapo mkutano huo unategemewa kumuidhinisha Bi
Hillary Clinton Kuwa Mgombea Urais wa Marekani kupitia Chama Hicho.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi