Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Makete kwa Wananchi wa Utweve Makete - Audio

Wananchi wa kijiji cha Utweve kata ya Ukwama wilayani Makete wameshauriwa kutosusia shughuli za maendeleo kijijini hapo na badala yake waendelee kuzifanya kama awali, wakati serikali ikishughulikia kero zao zinazowakabili

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Veronica Kesi wakati alipofika kijijini hapo kusikiliza kero za wananchi ikiwemo baada ya wao kutangaza kugomea shughuli za maendeleo kwa madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa shauri la kuuawa mtoto mmoja kijijini hapo na watuhumiwa wa mauaji hayo kupewa dhamana

Mh Kesi amesema anaungana na wananchi hao kuwapa pole kwa msiba huo uliowapata na kusema hoja zote zilizotolewa na wananchi katika mkutano huo amezichukua na kuahidi kwenda kuzifanyia kazi na wananchi kuona majibu kwa kuwa ziko hoja ambazo zipo ndani ya uwezo wake na nyingine zilizopo kwa upande wa mahakama watashirikiana na wataalamu wakiwemo wanasheria kuzitatua kisheria

Pia mkuu huyo amelaani mauaji hayo na kusema si vizuri mtu yeyote kujichukulia sheria mikononi na kusababisha kifo cha mwananchi yeyote
Sikiliza sauti hizi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo