Abiria waliokuwa wakisafiri na Basi la Princes Muro waisoma Namba

Abiria wanaosafiri kwa basi la Princes Muro lenye nambaya usajili T 551 DPQ lililoondoka Ubungo saa kumi na mbili alfajiri kuelekea Arusha, wamekwama  katika kituo cha mafuta cha Kibaha Madafu kuanzia saa moja na nusu asubuhi kwa madai kuwa limeharibika.

Mmoja wa abiria aliyejitambulisha kwa jina la STEVEN HENRY, ameiambia Redio One Stereo kwa njia ya simu kuwa tangu wakati huo hawaoni juhudi za matengenezo na wafanyakazi wa basi hilo akiwemo dereva na kondakta hawajulikani waliko.

Amesema wametoa taarifa ya mkasa huo kituo cha polisi Kibaha na askari wa usalama barabarani waliokwenda eneo la tukio, hawakuwaambia lolote wasafiri hao kuhusu hatua zinazochuliwa aidha zinazowapa au kuwaondolea matumaini  ya kuendelea na safari.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo