Henry Kilewo:Dar es Salaam ipo Chini ya Ukawa, Ndio Maana Analazimisha Serikali Kuhamia Dodoma

Nimesikia Mwenyekiti Mpya wa CCM Taifa ambaye alikuwa anagombea pekee ambaye pia alitangazwa na NEC kuwa Rais akisema atahamishia serikali yake Mkoani Dodoma kutoka Dar es salaam..

Ni kweli ni lazima serikali ihamie Dodoma kwakuwa Dar es salaam ipo chini ya Chadema/Ukawa na siyo CCM ndiyo maana analazimisha ihamie Dodoma.. Mkuu unasubiri nini? Ihamishie kesho maana Dar es salaam imewakataa ccm peleka sehemu ambayo Nec wamewatangaza...

Naelewa kuwa serikali kuhamia Dodoma ilikuwa ni adhima ya Mwl.Nyerere ila lilipouzwa kwakuwa Dar es salaam lilikuwa shamba la Bibi ila kwasasa kwakuwa Dar es salaam imeikataa CCM ni lazima Serikali ihamie Dodoma kama ambavyo imekuwa matakwa ya wengi na kupuuzwa... Tunakwenda kuichukua Dodoma 2020 na ndiyo mwisho wenu.....

Henry Kilewo
Katibu Greater Dsm (Chadema)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo