Msako wanaowapa mimba wanafunzi Dodoma, Angalia hapa

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana ameagiza kusakwa kwa wazazi wa wanafunzi 12 wa shule za msingi wilayani Bahi baada ya watoto wao kupata ujauzito. 

Akizungumza baada ya kumwapisha Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deogratius Ndejembi, Rugimbana aliwataka wakuu wa wilaya kupambana na tatizo la njaa katika wilaya zao ambalo linachangia wanafunzi wa kike kupata ujauzito. 

"Bado kuna upungufu mkubwa wa chakula katika baadhi ya maeneo na mahali panapoathirika zaidi ni kwenye elimu hasa kwa wanafunzi wa kike" alisema. 

Alisema mwaka huu Wilaya ya Bahi ina wanafunzi 12 wa Shule ya Msingi ambao wana ujauzito na amewaagiza watendaji wa wilaya hiyo kuwatafuta wazazi wao. 

Alisema wazazi wanawajibika katika malezi ya watoto wao na ndiyo maana ameagiza wasakwe.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo