Wananchi wa Ihela wakiwa kazini
Muonekano wa jengo la zahanati Kijiji cha Ihela
Wananchi wilayani Makete mkoani Njombe wametakiwa kuonesha ushirikiano
katika kutekeleza shughuli za maendeleo katika maeneo yao kwani kwa kufanya
hivyo kutasaidia kuharakisha maendeleo katika maeneo yao
Kauli hiyo imetolewa na wananchi wa kijiji cha Ihela kata ya
Tandala wilayani Makete wakati wakishiriki kufanya shughuli za maendeleo katika
zahanati ya kijiji hicho ambayo bado inaendelea na ujenzi
Wananchi hao walikuwa wakiongeza uwanja wa zahanati hiyo kwa kuchimba gema
lililopo jirani na zahanati ili kuweka uwazi, kazi ambayo waliisitisha kupisha
mwenge wa uhuru kuweka jiwe la msingi katika zahanati hiyo Juni 16 mwaka huu
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Soniphei Sanga amewashukuru wananchi hao
waliojitokeza kushiriki zoezi hilo na kuongeza kuwa wanatarajia kulikamilisha
ndani ya mwezi Julai mwaka huu na ndipo waendelee na shughuli nyingine za
kimaendeleo kijijini hapo