CHADEMA Mkoani Rukwa wasusia Mwenge

Chama cha demokrasia na maendeleo chadema mkoa wa Rukwa kimeunga mkono maamuzi yaliyotolewa na chama hicho makao makuu pamoja na yale yaliyokuwa yakifanywa na wabunge wa upinzani katika bunge lililomalizika hivi karibuni

Akizungumzia suala hilo mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Rukwa Sabriki Malila amesema hali na mwenendo wa kisiasa hapa nchini sio mzuri hali inayogandamiza demokrasia na mfumo wa vyama vingi

Naye katibu wa CHADEMA wilaya ya Sumbawanga Pius Ngurumali amesema viongozi na wanachama wa chama hicho hawatashiriki shughuli zozote za kiserikali ikiwemo zoezi la kuapishwa kwa wakuu wa wilaya pamoja na lile la mwenge wa uhuru unaotarajiwa kuingia mkoani humo kesho Julai 6 mwaka huu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo