Katika kuhakikisha mtoto wa kike anapata elimu katika mazingira safi bora
na salama shule ya Msingi Wanginyi wilayani Njombe imejenga choo maalum kwa
watoto wa kike waliopevuka wanachokitumia pindi wanapokuwa kwenye siku zao
Choo hicho kimejengwa wakati wa kampeni maalum ya ujenzi wa vyoo bora na
usafi wa mazingira kijijini na kwenye shule za msingi ambayo inafanyika kwenye
halmashauri 42 kote nchini chini ya uratibu wa wizara ya afya maendeleo ya
jamii jinsia wazee na watoto
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Ezra Mgaya anaeleza kuwa kabla ya kuanza kwa
utekelezaji wa kampeni hiyo hali ya mahudhurio ilikuwa hafifu kutokana na
matumizi ya choo cha mabanzi