DC azuia maandamano ya walimu

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Amani Mwenegoha amezuia maandamano yaliyoitishwa na Chama cha Walimu nchini (CWT) wilayani hapa, ambayo yalipangwa kufanyika leo kwa kuwa hayana msingi wowote. 

Mwenegoha ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya amesema hoja zote 17 ambazo waliziorodhesha walimu zilishajibiwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe kupitia barua yenye Kumb. Na. A.30/3/84 ya tarehe Mei 16, mwaka huu. 

Mkuu wa wilaya amekitaka chama hicho kama hakikuridhishwa na majibu hayo wakutane tena na mkurugenzi kuzungumzia masuala hayo, badala ya kufanya maandamano. 

Amesema maandamano hayo yataathiri shughuli za mitihani ya “mock” kwa kidato cha nne inayoendelea kati ya Mei 10 na Mei 20, mwaka huu na ile ya “Step” chini ya BRN kwa shule za sekondari iliyoanza Mei 16 na kukamilika Mei 20, mwaka huu. 

Amesema kamati ya ulinzi na usalama iko imara kuyadhibiti maandamano hayo na vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika wilaya hiyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo