Mama aua mtoto kwa viboko

Mkazi wa Kitongoji cha Majengo Kata ya Kabarimu Wilaya ya Bunda Mjini mkoani Mara anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumchapa mtoto wake Wakuru Rungu (9), viboko viwili kichwani na kumsababisha kifo. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Ramadhan Ng’anzi amesema tukio hilo lilitokea Mei 15 saa kumi na moja jioni baada ya mama huyo kumtuhumu mwanaye kuiba Sh8,000. 

Kamanda Ng’anzi amesema mtoto huyo ni mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Kabarimu. 

“Alimpiga sehemu ya kisogo hivyo kusababisha kupoteza mwelekeo,” alisema Ng’anzi. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo