Kidato cha 6 wamehitimu Mwakavuta Sekondari MAKETE, hapa kuna Picha 16

Mh Egnatio Mtawa
 
Halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imetoa kiasi cha shilingi milioni moja na laki tano kwa ajili ya ukarabati wa bweni katika shule ya sekondari Mwakavuta

Hayo yamesemwa na mgeni rasmi katika mahafali ya kidato cha sita katika shule hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa yaliyofanyika Ijumaa April 22 ambapo pamoja na mambo mengine amewasisitiza wanafunzi hao kufanya vizuri katika mitihani yao inayokuja na kuwa na moyo wa kusoma zaidi na zaidi ili wafike mbali kielimu

Pia ametoa wito kwa wananchi wa tarafa ya magoma kujitolea kukarabati BWENI LA shule hiyo kwa kuwa ni mali yao na shule hiyo inaendelea kuelimisha jamii bila ubaguzi wala upendeleo kama serikali inavyotaka

katika risala ya wahitimu hao iliyosomwa na Isaya Michael imetaja baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo kuwa ni pamoja na uchakavu wa mabweni hasa ya wasichana, ukosefu wa bwalo pamoja na uchache wa nyumba za waalimu

 Mwalimu akihojiwa na Mwandishi Dj Nundu




 Mkuu wa shule Mwakavuta

 Wanafunzi wahitimu wakiwa na Mkuu wa PCCB Makete



 Mwalimu nae akipokea zawadi

 Mhitimu akipokea cheti



 wahitimu wa kidato cha sita

wanafunzi waagwa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo