Tuhuma za ushirikina zimeibuka katika kijiji
Mnyawa halmashauri ya wilaya ya Tandahimba katika mkoa wa Mtwara ambapo wakazi
wake wanadaiwa kufanya vitendo hivyo dhidi ya wanafunzi ikiwa ni sehemu ya wao
kupinga wasifanye vizuri kwenye masomo yao
madai hayo yametolewa na mwalimu mkuu wa shule ya
Mnyawa Makeeja Maduhu baada ya tukio la hivi karibuni la wanafunzi zaidi ya 14
kukumbwa na ugonjwa wa ajabu wa kuanguka na kupoteza fahamu
Mashuhuda wa tukio hilo wanasema wanafunzi hao
walianza kuanguka majira ya saa moja wakati wakifanya usafi shuleni hapo
Mkuu wa wilaya hiyo Emmanuel Wahula amekemea
vitendo vya wananchi hao kukwamisha maendeleo ya elimu wilayani hapo