Wachina 13 wakamatwa mgodini Geita bila kibali

Idara ya uhamiaji mkoani Geita inawashikilia raia 13 wa China kwa tuhuma za kufanya kazi za kutafiti pamoja na kufanya kazi za kuchenjua madini ya dhahabu kinyume cha sheria.


Watuhumiwa hao wamekamatwa katika machimbo ya Igo katika kijiji cha Nyamahuna wilayani Geita kufuatia msako mkali kwa wageni wa mataifa kutoka nje wanaofanya kazi mkoani humo bila ya kuwa na kibali.

Akizungumza mara baada ya kuwakamata watuhumiwa hao afisa uhamiaji mkoa huo Charles Washima amesema watuhumiwa hao waliingia nchini kwa kibali cha matembezi lakini wamekuwa wakijihusisha na ufanyaji kazi kinyume na sheria.

Naye mmiliki wa mgodi huo Bi. Rehema Abdallah alishikiliwa na Idara hiyo baada ya kuhusika na kuwaleta raia hao wachina kufanya kazi katika mgodi wake bila ya kuwa na kibali maalum


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo