Taarifa Muhimu Kutoka Baraza La Mitihani Kuhusu Viwango Vya Ufaulu (Grade Ranges)

Baraza la Mitihani la Tanzania limekuwa likipigiwa simu na watu mbalimbali wakiomba ufafanuzi kuhusu taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa limebadilisha Viwango vya Ufaulu (Grade Ranges).

Baraza la Mitihani la Tanzania linapenda kuwajulisha watahiniwa na umma kwa ujumla kuwa taarifa hizo ni za UONGO na zinalenga kupotosha umma na kuleta taharuki. 

Hivyo, Baraza linaomba umma kuzipuuza taarifa hizo kwa kuwa Baraza halijafanya mabadiliko yoyote kuhusu Viwango vya Ufaulu vinavyotumika sasa. 

Imetolewa na,
AFISA HABARI NA UHUSIANO


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo