Mambo makubwa matatu aliyoyasema Mkuu wa wilaya ya Makete "LIVE" kwenye studio za 91.5 Green FM

Mkuu wa wilaya ya Makete Mkoani Njombe Daudi Yassin leo amefanya mahojiano maalum na kituo cha redio Green Fm 91.5 kilichopo wilayani hapo ambapo amezungumzia mambo mbalimbali ya kiwilaya na taifa kwa ujumla

Miongoni mwa mambo aliyoyazungumza ni pamoja na kukemea vitendo viovu na vya uvunjifu wa amani katika mkesha wa kuuaga mwaka 2015 na kuukaribisha 2016, na kuwataka wananchi wote wa Makete washerehekee kwa amani na utulivu

Suala jingine alilolisisitiza ni kuhusu hatua zitakazochukuliwa kwa wale wote watakaokiuka kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya wilaya yake kwa kuwa zoezi hilo ni endelevu

Sikiliza mahojiano hayo aliyoyafanya hii leo
Na hizi ni picha za Mkuu wa wilaya ndani ya studio za Green Fm 91.5 Fm
 Mkuu wa wilaya ya Makete Daudi Yassin akizungumza katika maojiano maalum ya moja kwa moja kwenye kipindi cha Drive home cha Green Fm


 Mkuu wa wilaya akijibu hoja mbalimbali


 Mtangazaji Edwin Moshi akimsikiliza mkuu wa wilaya akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo