Kaburi la Alphonce Mawazo laharibiwa

Zikiwa zimepita siku nne tangu aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo kuzikwa kijijini kwake Chikobe, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Salum Mwalimu amesema wamelazimika kuitorosha familia yake ili kunusuru maisha yao baada ya watu wasiojulikana kuvamia nyumbani kwake, kufanya fujo na kujaribu kuvuruga kaburi lake kwa kutawanya udongo. 

Mwalimu alisema jana kuwa wamelazimika kuitosha familia hiyo na kupelekea kuishi mahali ambako wana uhakika kuwa ni salama kwa maisha yao. 

Alisema watu hao baada ya watu hao kushindwa kuliharibu, waling’oa bendera za Chadema zilizokuwa zikipepea kwenye kaburi hilo na nyingine kwenye Jimbo la Busanda, huku wakiwapiga wafuasi wa chama hicho, akiwamo Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake (Bawacha) Mkoa huo, Husna Amred na kumjeruhi mwilini. 

Mwalimu alisema wakati Rais John Magufuli akifungua Bunge mjini Dodoma hivi karibuni aliwahakikishia Watanzania kuwa ataongoza nchini bila kujali itikadi ya vyama vya siasa, lakini yanayotokea mkoani Geita ni mambo ya kusikitisha na kutishia usalama wa maisha ya baadhi ya watu. 

Alidai kuwa kuna ya makundi ya vijana yanazunguka mitaani na kushambulia vijana wa Chadema ambao wanapaswa kukemewa kwa nguvu zote ili kulinda amani na utulivu. 

“Vitendo vinavyoendelea kutokea viongozi wa Chadema na wafuasi wao tunaelekea kuchoka kupigwa, kuuawa, kunyanyaswa na kunyimwa haki zetu … muda unakaribia sisi kunyanyuka endapo havitakomeshwa. 

Kamanda wa polisi mkoani Geita na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Ernest Mangu wasipuzie yanayoendelea kutokea kwani hayawezi kuvumilika na ni kinyume na sheria,” alionya Mwalimu. 

Polisi: Hatuna taarifa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Latson Mponjoli alisema hana taarifa za kutokea kwa fujo hizo nyumbani kwa marehemu Mawazo kijijini hapo wala kujeruhiwa kwa mtu yeyote na kuahidi kufuatilia kisha kutoa taarifa kwa vyombo vya habari. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo