Spika wa Bunge Job Ndugai awapa UKAWA onyo la mwisho

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Job Ndugai ameelezwa kusikitishwa kitendo kilichofanywa na baadhi ya wabunge kuzomea.

Amesema kitendo hicho siyo cha kiungwana na hivyo kulazimika kuwaomba radhi viongozi kutoka zanzibar na kuahidi kitendo hicho hakitajirudia tena.

Amesema wabunge waliomchagua wanaweza kumfanya awe spika mwema na mzuri 

Awali wakati wa kuwakaribisha viongozi mbalimbali akiwemo rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli na rais wa Zanzibar mh Dkt Ally Muhamed Shen ndipo viongozi hao wakaanza kupika kelele.


Wakati wa kumkaribisha rais wa zanzibar baadhi ya wabunge waliendelea kupiga kelele na hivyo kumlazimu spika wa bunge kuwataka watoke nje nao wakafanya hivyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo