Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk Hussein Kidanto (kushoto) akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru (kulia) ambaye ameteuliwa jana na Rais John Pombe Magufuli. Jana Rais Magufuli amemuamishia Dk Kidanto katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru ambaye ameteuliwa jana na Rais John Pombe Magufuli akizungumza na menejimenti ya hospitali hiyo jana.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma (MNH), Aminiel Aligaesha (kushoto) na mwanasheria wa hospitali hiyo, Veronica wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru.

Baadhi ya wakurugenzi wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru.
