Ajali ya basi yaua watu kadhaa huko Handeni Tanga

Watu watano wamekufa hapo hapo na wengine 39 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Matro walilokuwa wakisafiria kutoka Rombo kwenda Dar Es Salaam kuacha njia na kupinduka katika Kijiji cha Manga kata ya Mazingara wilayani Handeni. 

Akithibitisha taarifa hizo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Zuberi Mwombeji alisema kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa tano asubuhi jana katika kijiji hicho na kudai kuwa bado wanachunguza chanzo cha ajali ila inaonyesha ilimshinda dereva na kuacha njia

Kamanda Mwombeji alisema maiti watatu walitambuliwa na wengine wawili hawajatambuliwa bado na kuongeza kuwa majeruhi walikimbizwa hospitali kwa matibabu

Kamanda Mwombeji alisema dereva wa gari hilo hakuweza kupatikana ametoroka baada ya kutokea ajali hiyo. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo