Wanachama wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA wamefanya vurugu
kwenye ofisi ya msimamizi wa uchaguzi katika jimbo la Tabora Kaskazini kutokana
na kuwepo wagombea wawili wa chama hicho
Wagombea hao Daudi Nteminyanda aliyeshinda kura za maoni ndani ya chama
hicho na Joseph Kidaha aliyepitishwa na chama hicho makao makuu wamekutana
katika ofisi za msimamizi wa uchaguzi ambaye alikataa fomu ya Daudi na
kuzikubali za Joseph na kusababisha tafrani kwa wanachama wanaomuunga mkono
Nteminyanda
Mkurugenzi wa Uchaguzi jimbo la Tabora kaskazini Hadija Makwani amesema kwa
mujibu wa sheria zilizopo ofisi yake inamtambua Joseph Kidaha kwa vile
ametimiza vigezo na masharti ya kugombea nafasi hiyo
Mgombea ambaye alishinda kwenye kura za maoni Daudi Nteminyanda amesema
hakubaliani na maamizi hayo huku katibu wa jimbo hilo Lazaro mayani akisema
kuwa yeye amefuata taratibu za chama chake na hajakiuka