Breaking News: Waziri Mkuu wa Zamani, Fredrik Sumaye Aikimbia CCM Na Kuhamia UKAWA

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye ametangaza rasmi hii leo kujiondoa kwenye chama cha mapinduzi CCM na kujiunga na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA

Sumaye ametangaza uamuzi huo leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini DSM ambapo amesema anajiunga na UKAWA lakini ni chama kipi itakujulikana mbele ya safari

Amesema yeye kwenye CCM haondoki ili kukidhoofisha chama hicho, bali anaondoka ili kiimarike, maana yeye anajihisi ni mmoja kati ya makapi yanayotajwa na CCM

Sumaye amesema amefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na uvunjaji wa kununi  ndani  ya  CCM  ikiwemo katika harakati za kumteua mgombea wa Urais kwa upande wa CCM akidai mwenyekiti wa chama hicho Jakaya Kikwete alitumia ubabe katika kuwaingiza watu wake tano bora.

Huyu ni waziri mkuu wa pili kujiunga na vyama vya upinzani hapa nchini akimfuata Edward Lowassa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo