![]() |
KUTOKA Kilolo, upigaji wa kura za maoni katika jimbo hilo ulitaka kuingia dosari baada ya kuwepo kwa taarifa ya baadhi ya vituo kufunguliwa saa 12 asubuhi badala ya saa mbili.
Baadhi ya wananchi waliowahi katika vituo hivyo walipiga kura; kura zilizolalamikiwa na baadhi ya wagombea kwa madai kwamba zilipigwa mapema ili kumnufaisha mmoja kati ya wagombea waliotia nia katika jimbo hilo.
Katibu wa Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga alimaliza sintofahamu hiyo kwa kukubaliana na wagombea wote, kura zilizopigwa zihesabiwe ili kuthibitisha madai hayo.
