Uchaguzi wa kura zamaoni Waahirishwa baada ya kukamatwa karatasi zilizopigwa kura

Uchaguzi wa kura za maoni za  kuwatafuta wagombea ubunge na udiwani  katika  majimbo mawili ya Tarime  mkoani  Mara umehairishwa baada  ya kukamatwa  kwa karatasi  maalum za kupigiwa  kura zikiwa  tayari zimepigwa kwa  majina  yawagombea  wawili  katika majimbo hayo.

Akizungumza muda   mfupi  baada ya karatasi  hizo   kukamatwa,mwenyekiti  wa  CCM  wa wilaya  ya  Tarime Bw.Rashid Bugomba,amesema  zaidi  ya karatasi  elfu 20 zimekamatwa  zikiwa  na majina  ya  mh  gaudencia  kabaka wa jimbo la Tarime mjini na Mh. Nyambari  Nyangwine jimbo la Tarime  vijijini na kwamba wakati   tatizo hilo likitatuli ikiwa ni pamoja na kutafuta karatasi nyingine   za kupigia kura lazima uchaguzi huo  sasa usimamishwe kutokana   na   dosari   hizo.
 
Baadhi  ya wagombea katika  majimbo  hayo wamesema kuwa  ukiukwaji huo mkubwa wa uchaguzi  ndani  ya CCM umefanywa na   watu  wenye fedha  unaweza kuharibu kabisa zoezi zima la uchaguzi huo hata kama uchaguzi huo utahairishwa  endapo wagombea   hao  watarusiwa  kuendelea   na   zoezi   hilo.
 
Nao  baadhi  ya wapiga  kura wa katika uchaguzi huo wa kura za maoni  ndani  ya CCM  Wilayani Tarime wamedai hujuma  hiyo ni kubwa   imetengenezwa na baadhi ya watendaji  wa  CCM ngazi ya wilaya.
 
Hata  hivyo wagombea ambao  picha  zao  zinaonekana  katika    karatasi  hizo zikiwa tayari zimepgwa Mh.Gaudencia Kabaka na Mh.Nyambari Nyangwine wote kwa pamoja walipotafutwa kwa njia ya  simu kwa nyakati tofauti hawakupatikana kuzungumzia sakata  hilo  baada ya simu zao kuita kisha kizimwa na kwamba juhudi za  kuwatafuta bado zinaendelea.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo