Baada ya kura za maoni ndani ya chama cha mapinduzi CCM kwa ngazi ya Udiwani na Ubunge kufanyika hapo jana, wilayani Makete matokeo ya Ubunge bado hayajatangazwa rasmi
Kwa mujibu wa taarifa za mmoja wa kiongozi wa chama hicho wilaya ya Makete aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa madai kuwa si msemaji, matokeo hayo hayajatoka bado kutokana na kuendelea kuyakusanya hasa katika kata 7 ambapo kumeibuka utata
Hali hiyo imepelekea matokeo hayo kushindwa kutoka na mwandishi wetu bado anaendelea kufuatilia suala hili kwa ukaribu ili upate taarifa za uhakika na sahihi wa mamlaka husika
Aidha kumeendelea kuwa na mchuano mkali kati ya mbunge anayetetea nafasi yake Dkt Binilith Mahenge, na mgombea mwingine Prof Norman Sigala ambapo wamekuwa wakiongoza kwa nyakati tofauti katika matokeo ya awali kutoka kwenye kata mbalimbali
Endelea kufuatilia mtandao huu tutakujulisha
