Edward Lowassa amshushia tuhuma nzito rais Jakaya Kikwete

EDWARD Lowassa, mgombea urais wa Tanzania kupitia CHADEMA amesema, rafiki yake Rais Jakaya Kikwete ameharibu uchumi wa Tanzania.

Akizungumza na wafuasi wa Chadema pia UKAWA katika ofisi za Chadema mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania urais kupitia chama hicho amesema, 

“rafiki yangu Jakaya Kikwete ameuharibu uchumi wa nchi yetu,”
“Wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani kilo ya sukari ilikuwa Sh. 600 leo ni Sh. 2,300. Mchele ulikuwa Sh. 550 leo ni Sh. 2,300. Sembe ilikuwa Sh. 250 leo ni Sh. 1,200.”
Aidha Lowassa amesema, katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete ndipo wanyama wameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia ya Tanzania.
“Katika utawala wa Rais Kikwete, tembo wameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia duniani kote.
“Kila aina ya mnyama ameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia ya nchi yetu. Nitaijenga serikali yenye uchumi kwa speed (kasi), ambaye hawezi akae pembeni” 
amesema Lowassa.
Angalia video hii hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo