Mwanamke aliyeripotiwa kuwa kafa akutwa akiwa hai

Huko Ujerumani mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na miaka 92 ambaye aliaminika kupoteza maisha kisha mwili wake kuhifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti amezua gumzo.
Tayari daktari wa zamu alithibitisha kifo cha mwanamke huyo baada ya kumpima na kuridhika kuwa amefariki ..lakini baada ya masaa machache wahudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti walikuta mwili wa mwanamke huyo ukijigeuza na kugundua alikua hajafariki kama ilivyoripotiwa.
Tukio hilo lilifanya ndugu wa marehemu kushangazwa na hali hiyo huku wakimjia juu daktari aliyewapa taarifa kuwa mgonjwa wao amefariki duniani na kutaka walipwe fidia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo