Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) imesema kuwa kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa, haitaweza kufanyika tena tarehe 30 April hadi hapo itakapotangazwa tarehe nyingine tena.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mchana, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi , Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema sababu ya kuhairisha kura hiyo April 30 ni kutokana na kutokamilika kwa zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura kutokana na changamoto za mashine za BVR.
Jaji Lubuva amesema zoezi la uandikishaji mkoa wa Njombe litakamilika April 18 na baada ya hapo itafuatia mikoa ya Ruvuma, Iringa, Mtwara na Lindi . Vifaa vya kuandikishia (BVR kits) nyingine 248 zitawasili ndani ya wiki ijayo na vingine 1600 vitafuata baada ya muda mfupi.
Jaji Lubuva amesema zoezi la uandikishaji mkoa wa Njombe litakamilika April 18 na baada ya hapo itafuatia mikoa ya Ruvuma, Iringa, Mtwara na Lindi . Vifaa vya kuandikishia (BVR kits) nyingine 248 zitawasili ndani ya wiki ijayo na vingine 1600 vitafuata baada ya muda mfupi.
Pia, amesema kama vifaa vya kuandikishia vitafika vyote zoezi la uandikishaji litakamilka ifikapo mwezi julai mwaka huu.
Jaji Lubuva ameainisha kuwa Gharama za vifaa vyote vilivyoagizwa kwaajili ya vifaa vya kuandikishia (BVR kits) ni dola za Kimarekani milioni 72 ambazo ni sawa na Tsh bilioni 13,338,520,536
Jaji Lubuva ameainisha kuwa Gharama za vifaa vyote vilivyoagizwa kwaajili ya vifaa vya kuandikishia (BVR kits) ni dola za Kimarekani milioni 72 ambazo ni sawa na Tsh bilioni 13,338,520,536