Kwenye Hekaheka ya JANA ni tuhuma ambazo zinamhusu mwanamke anaedaiwa kuwa ni mke wa mwanajeshi, majirani na mashuhuda wengine wamesema mwanamke huyo amewaibia vitu mbalimbali.. hiyo tabia imewachosha.
Mjumbe wa eneo hilo amesema alipelekewa malalamiko mengi, akamfata mwanamke huyo kumuuliza lakini alikataa.. kijana mmoja amesema mama huyo alimuomba ampeleke kwenda kuflash simu, akamuahidi kama wakiiuza watagawana lakini hakujua kama simu hiyo ilikuwa ya wizi.
Baadae simu ilipatikana, lakini mama huyo amekataa kuhusika na wizi huo. Hekaheka itaendelea kesho na itafahamika jinsi ambavyo simu ilipatikana.
Kusikiliza Hekaheka yote bonyeza playa hapa chini…