MARAFIKI WA LOWASSA WAITIKISA SHULE YA MSINGI MWISENGE

Ukosefu wa vifaa vya kujifunzia pamoja na upungufu wa mabweni ya wavulana na wasichana kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum hasa kwa wanafunzi wenye Ulbinism katika shule ya msingi Mwisenge B ni moja ya changamoto kubwa ambazo zinaikabili shule hiyo shule ambayo amesoma baba   wa taifa hayati Mwl.Julius Kambarage  Nyerere katika kata ya Mwisenge manispaa ya  Musoma  mkoani Mara.

Mwalimu mkuu wa Shule hiyo Bw. Elias Makoro,amezungumza mara baada ya kupokea msaada wa  magodoro kutoka kwa  kikundi cha kijamii cha marafiki wa LowasSa kanda ya ziwa,kwa ajili ya   wanafunzi wenye mahitaji maalum,amesema ni vyema jamii na makundi mbalimbali ya kijamii  yakaendelea kutoa misaada mbalimbali ili kuweza kuwasaidia wanafunzi hao kusoma  katika mazingira mazuri na kuitaka jamii kutowatenga watoto hao.
 
Naye Bw.Edward Matiko,akisoma taarifa wakati wa kukabidhi msaada huo mkubwa,amesema wao kama  kikundi cha kijamii wameamua kutoa msaada huo wa magodoro kwa watoto  wenye Albinism katika  shule hiyo ili kuunga mkono matembezi ya kupinga changamoto zinazowakabili watu wenye Albinism  ambayo yaliongozwa na waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa  hivi karibuni pamoja kuunga mkono pia juhudi za mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dr.Reginald Mengi anazofanya katika kusaidia makundi  maalum katika jamii.
 
Awali kikundi hicho cha rafiki wa Lowasa wamefanya maandamano ya kilometa tatu kutoka musoma mjini hadi shule ya msingi Mwisenge  katika  kupinga vitendo vya ukatili na mauaji dhidi wa  watu wenye Ulbinism.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo