TINGA TINGA LABOMOA VIBANDA BARABARA YA MOROGORO DODOMA

Wakala wa barabara Tanroad mkoa wa Morogoro wamelazimika kutumia tingatinga kuvunja  vibanda na kuta za mabaa yaliojengwa  ndani ya maeneo ya  hifadhi ya barabara katika barabara kuu ya Morogoro Dodoma.

blog hii imehsuhudia baadhi ya wananchi wakibomoa na kuhamisha mali zao baada ya tingatinga kuanza zoezi la ubomoaji ambapo meneja wa Tanroad mkoa wa Morogoro Eng Doroth Mtenga amesema taratibu zote zimefuatwa ikiwa ni pamoja na kuwapa taarifa wananchi juu ya zoezi la uvunjaji  lakini walikaidi amri hiyo ambapo amesema zoezi hilo ni endelevu na hawatalipwa fidia yoyote  kuwataka wananchi wengine waliojenga ndani ya mita 22.5 katika hifadhi ya barabara kuu ikiwemo ya barabara ya Morogoro Dar es Salaam na Morogoro Iringa kuvunja kwahiari ili kupisha shughuli za maendelezo ya barabara pamoja na usalama wa wananchi wenyewe.
 
Kwa upande wao wananchi waliovunjiwa vibanda  na kuta wakiwemo wamiliki wa mabar wakizungumzia uvunjaji huo wamekiri kuwa walipewa taarifa za uvunjaji na wengine wakiiri kujenga katika hifadhi ya barabara ambapo baadhi ya wakazi wa mkoa wa morogoro wamepongeza hatua iliochukuliwa na wakala wa barabara Tanroad  kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kutaka kupata faidha bila kujali usalama wa wananchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo