SOMA KILICHOMUUA ABDUL BONGE MWANZILISHI WA TIPTOP CONNECTION

Saa zinahesabika toka Tanzania na familia ya bongofleva ipokee taarifa za msiba wa Abdul Bonge Mwanzilishi wa kundi maarufu la Bongofleva Tiptop Connection lenye wanachama kama Tunda Man, Madee, Dogo Janja na wengine waliopita kama Keisha, Cassim Mnganga na MB Dogg.
Jioni ya March 28 2015 ndio taarifa zilianza kusambaa lakini chanzo cha kifo cha ghafla cha Abdul hakikuwa kimesemwa lakini mdogo wake ambae ni Babu Tale ameongea na kusema >>> ‘Kuna mshkaji wetu mmoja alikua anagombana na mke wake jirani yetu, wakamfata hapa Abdul aende… mara ya kwanza na ya pili akakataa, mara ya tatu akasema ngoja aende’
Abdu Bonge na Bab TaleAlivyoenda ukapita ukimya kidogo, baadae kuna mtu akaja kumuita kaka yetu mkubwa mwingine na kumwambia nenda kamsaidie kaka yako mkubwa amedondoka, kaka yangu baadae akanipigia simu akasema Bonge kama amezimia lakini sidhani kama atapona sababu wakati wa kuamulia ugomvi alianguka baada ya kusukumwa nafikiria aliangukia kichogo, kumpeleka Hospitali Manzese wakasema ameshafariki‘ – Babu Tale.
Taarifa kutoka msibani March 29 2015 zinasema Abdul atasafirishwa kwenda kuzikwa Morogoro baada ya mwili kuzuiliwa leo mpaka uchunguzi ukamilike, kwa sasa Watu mbalimbali wakiwemo wasanii wa bongofleva wako Tiptop Manzese kwenye kutoa pole, mwili unatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda Morogoro.
Naambiwa maziko yatafanyika kijiji cha Mkuyuni Morogoro, kwa asiyepajua Mkuyuni ni njia ya kwenda Matombo. #RIP #AbduBonge

CREDITS:MILLARDAYO.COM


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo