Mama huyo aliyetoa zawadi alikuwa akisambaza taarifa kwamba alitoa zawadi kitambaa cha sare ya nguo ya shule kwenye sherehe ya mtoto wa mama huyo mwingine, lakini mama wa mtoto huyo hakumtuza vitu vya thamani kama ambavyo yeye alitoa.
Mama huyo amesema rafiki yake alimtaarifu kuhusu sherehe ya mwanae lakini akamwambia hana kitu kwa muda huo kwa ajili ya kuandaa zawadi, akampelekea zawadi ya kitambaa lakini baadae akapata taarifa kwamba anatangazwa kwamba hana fadhila.
Alipopata taarifa za maneno hayo aliamua kununua vitu alivyopewa zawadi hizo na kukodi ngoma ya mdundiko kwa ajili ya kwenda kumrudishia, alipofika nyumbani kwake mwanamke huyo hakutoka ndani, akaamua kukabidhi vitu hivyo kwa majirani ili akitoka wampatie.
Bonyeza play hapa chini kusikiliza Hekaheka yote…