WAZIRI MKUU PINDA ADAI YEYE NI MWADILIFU NA HAJAWAHI KULA RUSHWA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema yeye ni mtu mwadilifu ambaye hajawi kutoa wala kupokea rushwa kwa mtu katika maisha yake yote.

Pinda amesisitiza kwamba ana hakika kuwa hata siku moja hawezi kukamatwa kwa kosa la kupokea rushwa,isipokua kuna watu wanamchafua mara baada ya kutangaza nia yake ya kuvaa viatu vya Rais Kikwete.

Alisema kuwa wako baadhi ya watu walipanga kumchafua kwa kutaka kumsingizia wakati wa mkutano wa 16 na 17 Bungeni kwamba anahusika na uchotwaji wa fedha za Escrow.

“Nilishangaa sana watu ambao walitaka kunichafua kwa kunihusisha na fedha za Escrow,mimi sihusiki na wala sitahusika hata siku moja katika kupokea na kutoa rushwa mahali popote pale”alisisitiza Pinda.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo