MAMA AMCHOMA MOTO MWANAYE, KISA KADOKOA VIPANDE VIWILI VYA NYAMA

Mwanafunzi wa Darasa la pili katika shule ya msingi Ungindoni kata ya Mji mwema Dar es salaam anadaiwa kuchomwa moto na mama yake mkubwa sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kutumia jalo.

Mtoto huyo alifanyiwa ukatili huo siku ya krismasi akidaiwa kula vipande viwili vya nyama na hivyo kupewa adhabu na mama yake huyo kwa kuchomwa moto kwenye paja,mikono,magoti na miguu.

Mmoja wa shuhuda wa tukio hilo alisema  majirani walibaini kujeruhiwa kwa mtoto huyo mara baada ya kutoka nje na kuonekana akichechemea na alipoulizwa alisema amechomwa na na mama yake huku akionyesha maeneo alikofanyiwa ukatili huo.

Mama mkubwa Rachel alipoulizwa sababu ya kufanya hivyo alisema alichukua uamuzi huo baada ya kubaini alikula mboga na alipoulizwa alikana.

“Nakiri nimekosea kimpiga lakini mara kwa mara nimekua nikimuonya aache tabia ya wizi lakini amekua hasikii”alisema Rachel.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo