WAGONJWA WATELEKEZWA HOSPITALI YA MUHIMBILI NA NDUGU ZAO

Ofisa uhusiano wa Taasisi ya MOI, Frank Matua amesema jumla ya wagonjwa nane wametelekezwa katika taasisi hiyo na ndugu zao baada ya kutibiwa na kujikuta hawana kwa kwenda.

Matua amesema kati yao wapo wagonjwa ambao wamekaa kwa zaidi ya miaka miwili, wengine mwaka mmoja na wengine miezi zaidi ya miwili ambao walifikishwa kutibiwa baada ya kupata ajali ya barabarani.

Ofisa huyo amesema wengine wana matatizo ya akili, hawawezi kujieleza hivyo ni ngumu kupata taarifa zao, hawawezi kuwaruhusu wakaondoka na kuzagaa mitaani hivyo wanalazimika kuendelea kuwa nao hapo hospitalini kwa muda wote wakisubiri ndugu zao kujitokeza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo