Ofisa uhusiano wa Taasisi ya MOI, Frank Matua amesema jumla ya wagonjwa nane wametelekezwa katika taasisi hiyo na ndugu zao baada ya kutibiwa na kujikuta hawana kwa kwenda.
Matua
amesema kati yao wapo wagonjwa ambao wamekaa kwa zaidi ya miaka miwili,
wengine mwaka mmoja na wengine miezi zaidi ya miwili ambao walifikishwa
kutibiwa baada ya kupata ajali ya barabarani.
Ofisa huyo amesema wengine wana matatizo
ya akili, hawawezi kujieleza hivyo ni ngumu kupata taarifa zao,
hawawezi kuwaruhusu wakaondoka na kuzagaa mitaani hivyo wanalazimika
kuendelea kuwa nao hapo hospitalini kwa muda wote wakisubiri ndugu zao
kujitokeza.