MKURUGENZI WA HALMASHAURI ALIPUKIWA NA BOMU, POLISI WATHIBITISHA

Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Iramba Singida, Halima Mpita amenusurika kifo baada ya kulipukiwa na kitu ambacho kinadhaniwa kuwa bomu la kutengenezwa kienyeji.

Kamanda wa Polisi Singida, Thobias Sidoyeka amethibitisha kutokea kwa tukio hilo nyumbani kwa Mkurugenzi huyo wakati akijiandaa kwenda kazini, mlipuko huo ulitoka kwenye bahasha ambayo aliipokea juzi kutoka kwa Katibu Muhtasi wake.

Ndani ya bahasha hiyo kulikuwa na ujumbe “Poleni sana, hatuwezi kufanya dili la milioni 90 halafu mkala peke yenu, sisi mkatudhulumu tukawaacha”, baada ya kuisoma alienda nayo nyumbani bila kujua kama kuna kitu kingine ndani.

Wakati akijiandaa kwenda kazini siku ya jana ndipo mlipuko huo ulipotokea, hakuna aliyekamatwa ila Polisi wanaendelea na upelelezi wakishirikiana na JWTZ ili kubaini kama mlipuko huo ulitokana na bomu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo