Simba wanne waliotoka nje ya hifadhi ya Taifa ya Tarangire na kuingia
eneo la kijiji cha Kibaoni, Manyara wameuawa kwa kuchomwa mikuki na
wananchi.
Kijiji hicho kipo hatua chache kutoka ndani ya hifadhi hiyo ambayo ni
mojawapo ya vivutio vya utalii wa Tanzania na mara nyingi wayamapori
huzagaa mitaani hasa kipindi cha masika kuepuka majani marefu hifadhini.
Tukio hilo ambalo lilielezwa kuw ani janga kubwa katika sekta ya
utalii nchini,lilitokea jana alfajiri hadi saa 6 mchana na mizoga saba
ya Simba ilipatikana huku mmoja akiaminika kufia kwenye vichaka baada
ya kukimbia alipojeruhiwa.
Waziri wa Maliasili Lazaro Nyalandu ameziagiza mamlaka zinazohusika
kuwasaka na kuwatia mbaroni wahusika kuwaongoza wanakijiji hao kuua
Simba hao kinyume na utaratibu.
