ASKOFU AELEZEA ALIVYOPEWA MGAWO WA FEDHA ZA ESCROW

Askofu msaidizi wa kanisa jimbo kuu Dar es salaam Eusebius Nzigilwa amevunja ukimya kuhusu mgao wa sh.milioni 40.4 alioupata kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya VIP Engineering& Marketing limited James Rugemalira.

Ukimya wa askofu Nzigilwa unatokana na sakata la uchotwaji wa zaidi ya bilioni 300 kutoka katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyokua katika benki kuu ya Tanzania BoT.

Alisema kiutaratibu siyo vibaya waumini kutoa michango na matoleo kwa kanisa na watumishi wake.

Alisema aliombwa akaunti yake na Rugemarila mwanzoni mwa mwezi Februari na kwamba hakuwahi kufahamu kiasi cha fedha kilichowekwa kwenye akaunti yake hadi alipoangalia taarifa ya benki Februari 27 iliyoonyesha aliingiziwa milioni 40.4.

“Niliwasiliana na Rugemarila na kumwambia nimeona kiasi kikubwa cha fedha katika akaunti yangu,naye akaniambia hayo ni matoleo yake ambayo anaamini yatasaidia katika shughuli za kitume na kiuchungaji,,nikamshukuru kwa ukarimu huo mkubwa”alisema askofu huyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo