WAZIRI NYALANDU NAYE ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS MWAKANI

Mbio za urais ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM  zimechukua sura mpya baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu  kutangaza rasmi kuwania kiti hicho mwakani.

Akizungumza katika mkutano wa kuwashukuru wapigakura wake Mkoani Singida alisema muda Tanzania kupata maono mapya umefika.

“Muda wa Tanzania kupata maono mapya umefika,nitachukua hatua ya kuelekea Dodoma kuchukua fomu muda ukifika,maelfu ya watu watanisindikiza wanaume,wanawake,vijana kutoka Mikoa mbalimbali.

“Wale wote waliotangaza nia kupitia chama changu kazi zao lazima zipimwe kwa moto na zianikwe hadharani ili mwisho wa siku CCM yenyewe itazipima”alisisitiza.

Alisema pindi Rais Kikwete atakapohitimisha utawala wake, lazima atakabidhi kijiti kwa kizazi kipya.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo