SERIKALI KUTANGAZA MAJINA YA WAFANYAKAZI WA TRL WATAKAOFUKUZWA KAZI WIKI IJAYO

Waziri wa Uchukuzi Dk.Harrison Mwakyembe amesema wiki ijayo atatangaza majina ya wafanyakazi wa kampuni ya Reli Tanzania TRL watakaofukuzwa kazi kutokanana kutokua na tija kwenye kampuni.

Aidha alisema huduma ya usafiri wa Reli ya kati,zitaanza mwishoni mwa mwezi wa Januari hivyo kuwataka wananchi wanaoishi kandokando ya Reli kuondoka kwani wanahatarisha maisha yao.

“Serikali inawekeza ili tuone tija,na kama tija haionekani basi uongozi wa juu una shida,hatuwekezi pesa na kunyima sekta nyingine halafu reli ikabaki vile vile,fanyeni kazi kwa ubunifu la,nitafukuza wote”alisema Mwakyembe.

“Shirika limejaa mtandao wa wezi tuukiwemo wa mafuta,nimewaonya iliyopita,kazi yenu wizi tu na kulifanya Shirika likose tija,leo tunaleta vifaa vya mabilioni ya kodi za wananchi,kichwa kimoja cha treni kinagharimu bilioni 7,halafu kinapinduka kwa uzembe uzembe tu”alisema.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo