WAFANYAKAZI WA ATCL WAIPELEKA SERIKALI MAHAKAMANI, KISA MADENI

Waliokua wafanyakazi wa Shirika la ndege ATCL wamefungua madai ya kuomba kukazia hukumu katika mahakama kuu ya Tanzania kitengo cha Kazi,wakiomba kukamata na kuliuza jengo la ATC House ili wafidie malimbikizo ya mishahara yao.

Kwa mujibu wa madai hayo namba 385 ya mwaka 2014 kupitia wakili wao Benjamini mwakagamba,pia waliomba mahakama hiyo kuteua dalali  atakayeliuza jengo hilo lililopo eneola Posta.

Mmoja wa wafanyakazi hao kapteni Suel Mjungu alisema anadai sh.72,757,042.48 huku mwenzake Msami akidai  sh.114,244,807.3 ambazoni za awamu ya kwanza walitakiwa kulipwa Oktoba 2013 lakini hadi sasa hawajalipwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo