WANAUME WANAOFANYIWA UKATILI MKOANI RUVUMA WAANZA KUJITOKEZA



Matukio ya wanaume kunyanyaswa na kufanyiwa ukatili na wake zao ikiwemo kumwagiwa maji ya moto na hata wengine kukatwa viungo vyao yameshika kasi mkoani Ruvuma ambapo baadhi ya wanaume wameanza kuripoti matukio ya kunyanyaswa na wake zao katika madawati ya Jinsia.
 
Hayo yameelezwa na wanaharakati wa haki za binadamu kwenye kongamano la maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia lililoandaliwa na shirika la kuhudumia watoto yatima Ruvuma (ROA) la Mkoani Ruvuma.
 
Akifungua kongamano hilo mkuu wa wilaya ya Songea Bw. Joseph Mkirikiti amewataka wanawake kuwafundisha mabinti kuheshimu ndoa zao ili kukomesha unyanyasaji huo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo