Hussein alisema jana kuwa kiongozi huyo atadondoka gafla kwenye jukwaa na kufariki dunia wakati akipelekwa hospitali.
Alisema pia mwandishi mmoja mashuhuri nchini pia atakufa kifo chenye
utata kitakachoitesa Serikali na familia yake katika kutafuta sababu za
kifo chake.
Kuhusu uchaguzi Mtabiri huyo alisema kundi la vijana na wazee nyota
inaonyesha kwamba watakaofaidika ni vijana lakini kuna wazee pia
watakaoweza kufaidika ambao ni wale wenye sura za 'babyface' au wenye
kupenda mambo ya ujana.
Alisema ili Tanzania ilinde sifa ya kuwa nchi yenye kuwa na amani na
utulivu ni kuwa na rais kijana mwenye mchanganyiko wa dini mbili au
mwenye ndoa ya dini tofauti.