MKOA WA NJOMBE WATAJWA KUWA MIONGONI MWA MIKOA ILIYOFANYA VIZURI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

CCM Yaongoza Uchaguzi Wa Serikali Za MItaaMatokeo ya Jumla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14 mwaka huu, yanaonesha Chama cha Mapinduzi kimepata ushindi katika  vijiji 7,290 Kati ya vijiji 9,290 vilivyokwishatangaza matokeo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana  Mjini Dodoma   Mkurugenzi wa Uchaguzi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Khalisti Luanda  alisema, katika matokeo hayo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepata vijiji 1,248, chama cha  TLP vijiji viwili, chama cha  NLD viwili,  UDP vijiji vinne na chama cha   CUF kilipata ushindi katika  vijiji 949.

Akitangaza matokeo ya Mitaa Khalisti alisema, Kati ya Mitaa 3,078 ilitoa matokeo , CCM imeshinda katika Mitaa 2,116,Chadema Mitaa 753,
CUF Mitaa 233,NCCR-Mageuzi Mitaa nane,TLP Mtaa mmoja,na ACT Mitaa tisa
Vyama vingine ni UMD, UDP na NRA kila kimoja  kimeshinda  Mtaa mmoja.

Khalisti alisema matokeo ya  maeneo yote yaliyofanya uchaguzi Desemba yantarajiwa kutangazwa leo ambayo ni siku ya mwisho.

Aidha   Mkurugenzi huyo aliitaja  mikoa 11 ambayo imetekeleza uchaguzi vizuri kuwa ni  Arusha, Dodoma, Mbeya, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Katavi, kagera , Iringa na Njombe.

Na Mikoa ambayo uchaguzi haukufanyika kwa ufanisi ni  Kigoma, Tabora, na  Pwani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo