Taarifa zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed
Msangi zilieleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa nane mchana
katika mteremko wa Kanyegele, Kata ya Ntokela wilayani Rungwe.
Kamanda Msangi alisema lori hilo aina ya Mitsubishi Fuso yenye namba
za usajili T143 ACR lilikuwa likitokea Ilemi jijini Mbeya likiwa
limebeba maiti na waombolezaji kuelekea wilayani Rungwe.
Alisema baada ya kufika katika mteremko wa Kanyegele dereva wa gari
ambaye hakufahamika jina lake mara moja alipojaribu kulipita gari
lililokuwa mbele yake ghafla lilijitokeza gari jingine mbele yake na
alipojaribu kuminya breki lilimshinda na hatimaye kutumbukia kwenye
korongo na kusababisha vifo na majeruhi hao.
Alisema kati ya majeruhi 36, wawili walikimbizwa katika Hospitali ya
Rufaa Mbeya kutokana na hali zao kuwa mbaya zaidi, tisa wakapelekwa
hospitali ya Wilaya ya Rungwe ya Makandana na 25 walipelekwa katika
kituo cha afya Igogwe