MWANADADA anayefanya vizuri katika muziki wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura 'Lady Jaydee' amesema kamwe hatarajii kujiingiza katika masula ya siasa kama wanavyofanya wanamuziki wenzake.
Kauli
hiyo aliitoa wakati akizungumza na waandishi wa habari wa gazeti la
Jambo Leo Dar es Salaam jana, baada ya kutembelea chumba cha habari cha
gazeti hilo katika Jengo la Hifadhi House katika makutano ya Barabara za
Azikiwe na Samora.
"Binafsi
sitarajii kuingia katika masula ya siasa mimi nitaendelea na muziki na
hao wenzangu waliojiingiza katika siasa ni utashi wao."
Alisema
anafurahi kufanya muziki na wala hajuti kwa kuwa unamuongezea
kipato,kikubwa ni kutunga nyimbo zenye maudhui na mvuto na kwa wakati
husika.
Baadhi
ya wanamuziki waliojiingiza katika siasa ni Joseph Mbilinyi 'Sugu'
ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), Joseph Haule 'Profesa J, Khadija Shabani 'Keisha'
Ummy Wenslaus 'Dokii, na wengine kama Fullgence 'Mwanacotide' ambaye
yupo Chadema.
