Mrembo na mwigizaji wa filamu hapa Bongo, Coletha
Raymond ‘Koletha’ amefunguka kwamba tangu aingie kwenye fani hiyo
hajawahi kuwa na mpenzi msanii na hapendi hata kuwasikia.
Akipiga stori na mwandishi, Koletha alisema kutokana na kwamba
anazijua tabia zao kwani anafanya nao kazi pia wakati alipoanza fani
hiyo alijiapiza kwamba hatakuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu
anayefanya naye kazi.
“Sijawahi kutoka na msanii na siwezi kutoka nao kimapenzi kwa sababu
ni kitu ambacho nimejiapiza halafu pia inapunguza ufanisi wa kazi hivyo
sina hata wazo la kuwa nao kwa kweli, mimi huwa nakuwa na uhusiano na
watu wa kawaida,” alisema Koletha.
GPL