MWALIMU AWATAKA WANANCHI KUSOMA KATIBA PENDEKEZWA ILI WAJUE MAZURI NA MABAYA KWANZA

Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema kimewataka watanzania kujiwekea utaratibu wa kuisoma katiba inayopendekezwa ili kuelewa yaliyondani ya katiba hiyo kwa lengo la kugundua mazuri na mabaya yaliyo ndani ya katiba hiyo pendekezwa badala ya kutegemea kusikia kutoka kwa wanasiasa ambao wanaweza kuwadanganya kwa lengo la kulinda maslahi yao ya kisiasa.

Naibu katibu mkuu wa Chadema Zanzibar Salum Mwalimu ametoa wito huo wakati akiwahutubia wakazi wa tarafa ya idodi mkoani Iringa ambapo amesema katiba hiyo inayopendekezwa ina mapungufu mengi na imetungwa kwa kuzingatia maslahi ya kundi fulani la wanasiasa ambapo licha ya kuwanyima wananchi nguvu ya kuiwajibisha serikali pia imeliondolea meno hata bunge la jamhuri kuisimamia serikali.
 
Kwa upande wake mbunge wa Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa amewataka wabunge wa mkoa wa Iringa kuunga mkono juhudi zake za kuitaka serikali kuujenga uwanja wa ndege wa nduli mkoani Iringa katika kiwango cha kimataifa ili kusaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi ya taifa ya ruaha ambayo ndiyo ya pili kwa ukubwa barani afrika lakini ikiwa nyuma kimapato kulinganisha na hifadhi nyingine za ukanda wa kaskazini.
 
Naye mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Iringa Mustapha Msowela amewataka wananchi kujiandikisha katika daftarai la makazi na lile la kudumu la wapiga kura ili waweze kuchagua viongozi wanye nia ya kuwatumikia katika chaguzi zijazo huku makamu mwenyekiti wa baraza la vijana la chama hicho Patrick Sosopi akiwataka wananchi hao kutochagua viongozi wanaotokana na rushwa kwenye vyama vyao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo