TRA KUANZISHA MFUMO MPYA WA ULIPAJI USHURU WA FORODHA MPAKA WA TUNDUMA

NA KENNETH NGELESI,MBEYA
MAMLAKA ya Mapato nchini ,TRA, kitengo cha ushuru wa forodha imeanza kutoa mafunzo kwa Mawakala wa Forodha na Watumishi wa Idara ya Forodha mikoani  juu ya matumizi ya mfumo mpya wa utoaji wa mizigo kwa kasi katika Bandari na Mipaka ya nchi.

Mfumo huo unaujulikana kama (TANCIS) unakuja badala ya ule wa zamani (ASYCUDA) na ukiwa mpango ambao umelenga kupunguza msongamano wa magari ya mizigo mipakani, kuharakisha malipo ya ushuru na hivyo kuongeza kasi ya kukua kwa uchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Tunduma
Meneja Msaidizi wa TRA Mkoa wa Mbeya kitengo cha ushuru na Forodha Joseph Ruge alisema wanatoa mafunzo kwa watumishi 40 wa mamlaka hiyo na Mawakala 60 kutoka mpaka wa Tunduma na kwamba umelenga kuwafikia Mawakala 1000 kutoka Mikoa ya Tanzania.

Ruge alisema kuwa mfumo huo ni kimtandao zaidi kwani mteja ama wakala anaweza kufanya hatua zote na utoaji wa mzigo kutoka Bandari ya Dar-es-salaamu akiwa nyumbani kwa kutumia simu ya Mkono imradi kuwe na mtandao.

Alisema kuwa mfumo huo ulianza kufanyiwa utafiti April mosi mwaka huu kwa kushirikiana na watanzania na nchi ya  Korea, ambapo Julai Mosi umeanza kufanyakazi katika bandari ya Dar-es-salaam.
Akizungumza uamuzi wa kutoa elimu kwa  mawakala katika Mpaka wa Tunduma na si mikoa mingine Ruge alisema kuwa kutokana na umuhimu wa mpaka huo ambapo asilimi 70 ya mizigo inayo pakuliwa katika bandari ya Dar-es-salaam inapitia mpaka huo kwenda nchi karibu zote za kusini mwa Jangwa la Sahara.

Kwa upande wake Sigsimund Kafuru Ofisa elimu na huduma kutoka Makao Makuu ya TRA Muwezeshaji katika Mafunzo hayo  Hilda mponzi walisema kuwa mfumo huo unafaidi kubwa kwani ni wa uwazi na utaondoa udanganyifu katika masuala yote ya upakuaji wa mizigo.

Alisema kuwa  kumekuwa nan tabia ya udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na vishoka ama wafanyakazi wasio waaminifu juu kiwango cha malipo, na hatua ulipo fikia mzigo lakini kwa kufanya hivyo mteja anaweza kujua malipo pamoja na hatua ulipo fikia.

‘Yahani mfumno huu utaondoa kabisa watu wanao jiita vishoka kwani wamekuwa wakiwa tanganaya wateja juu,malipo pamoja na hatua ulipo fika mzigo lakini kwa njia hii mteja anaweza kungalia kupitia mtandao na akafahamu mzigo upofikia katika hatua ipi na malipo ni kiasi gani?’alihhoja Mponzi

Katika hatua ngingine Mponzi aliongeza kuwa faidi nyingine ya kutumia njia hiyo ni kushirikisha tasissi zote ambazo zimekuwa zikihusika katikia usarishaji na upakuji wa mizigoi ikiwe shirika na viwango (TBS),Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TRFA) ambapo taarifa zote zitafanyika kwa wakati mmoja.

Baada ya Dar es salaam ambapo mfumo huu umeanza kutumika Julai mwaka huu, TRA inautambulisha mfumo huu kwa Mawakala wa forodha wa Mpaka wa Tunduma mkoani Mbeya na hii inatokana na mpaka huu kuwa na msongamano mkubwa wa Magari ya mizigo ikilinganishwa na mipaka mingine nchini.

Meneja Msaidizi wa wa Forodha, TRA, Mkoa wa Mbeya Joseph Ruge na mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo,Hilda Mponzi wanazungumzia mfumo huo unavyofanya kazi kwa kuzihusisha pia Idara nyingine za serikali

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo David Okechi ambaye ni mwenyekiti  Mwenyekiti wa Makampuni ya Wakala Tanzania alisema kuwa mfumo huyo utakuwa mkombozi kwao kwani utapunguza mizunguko ya mara kwa mara na kwamba hatu zote za kupitisha mzigo zinaweza kufanyika akiwa ofisini.

 ‘Katika hali ya kawaida ni wazi kuwa mfumo huu utatupunguzia mizunguko isiyo ya lazima kwani  kwa sasa tunazunguka ofisi zote ili kupitisha mizogpo yetu lakini kwa mfumo huu mpya taarifa zote tutazipata na kujaza kutia mtandao’alisema


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo