Mtangazaji wa redio na rapper mkongwe, Anselm Ngaiza aka Soggy Doggy
amehamia kwenye kituo cha redio cha EFM cha Dar es Salaam akitokea Ebony
ya Iringa.
Soggy amefanya kazi kwa miaka kadhaa akiwa kama mkurugenzi wa vipindi wa
Ebony FM hiyo inayosikilizwa zaidi kwenye mikoa ya nyanda za juu za kusini.
Rapper huyo ametweet:
Thanks
kwa kila aliyenipa ushirikiano nikiwa Ebony FM Iringa,maisha yanaenda
kasi sana na kuna vitu havikwepeki nimeamua kuhamia 93.7 Efm
Soggy amewahi kufanya kazi kwenye vituo vingine vya redio vikiwemo
Triple A ya Arusha na Radio Free Africa ya Mwanza.
